Tuesday 25 September 2012

CHADEMA: Kama safari ya kifisadi RC atushitaki

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Manispaa ya Moshi kimemtaka Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, kutumia vyombo vya ulinzi na usalama kuwakamata na kuwashitaki madiwani kwa kile anachodai ufisadi uliotaka kufanywa na madiwani hao katika safari yao ya mafunzo Kigali nchini Rwanda.
CHADEMA kupitia makada wake maarufu, James ole Millya na Jafary Michael walitoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati wa mikutano ya hadhara iliyoanza hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi kutoa ufafanuzi kwa wananchi wa hatua ya mkuu huyo wa mkoa kuzuia safari hiyo huku wakiita ni ya kisiasa zaidi.

Mapema mwezi huu, Gama aliwaambia waandishi wa habari mbele ya kamati ya ulinzi ya mkoa kuwa amesitisha safari hiyo ambayo ingegharimu sh milioni 123.2.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Penford vilivyoko katikati ya mji wa Moshi, Meya wa manispaa hiyo, Jafary Ally, alisema fisadi yeyote anapothibitika anachukuliwa hatua za kisheria.

“Ndugu zangu wananchi wa Moshi, kama kweli Gama anaona kile madiwani wa CHADEMA walichotaka kukifanya ni ufisadi….. leo hii hakuna hata mmoja wetu ambaye angekuwa katika eneo hili la mkutano, wote tungekuwa gerezani.

Alisema mkuu huyo wa mkoa sasa ameacha majukumu yake ya kiserikali na kuanza kutumika kisiasa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa lengo la kuwagombanisha madiwani hao ambao wengi wao wanatoka CHADEMA.

Meya Michael alisema fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo madiwani zitatumika kama zilivyopangwa na kama mkuu huyo wa mkoa akiendelea kutumika kisiasa na kuacha shughuli za utendaji wa kuwatumikia wananchi, watatangaza mgogoro naye wa kutoshirikiana kwenye shughuli zozote.

Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU